Dk. Camillus Kassala mtoa mada
Na Elias Mhegera
Imetabiriwa kwamba mara ifikapo mwaka 2017
Tanzania itarejea katika kulitambua rasmi Azimio la Arusha bila kujali rais
atatoka katika chama tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM) au upinzani.
Utabiri huo ulifanywa na mwanazuoni maarufu
katika masuala ya uchumi, siasa na falsafa Dk. Camillus Kassala alipokuwa akitoa mada kuhusu uchumi wa soko unaozingatia
mahitaji ya jamii.
Alikuwa akitoa mada kwa wanafunzi wa chuo cha
Mwalimu Nyerere Kivukoni waliokuwa katika maandalizi ya ziara ya mafunzo nchini
Ujerumani. Siku ya Ijumaa tarehe moja, Agosti, 2014.
Wanafunzi kutoka chuo hicho na wale wa
Ujerumani wamekuwa katika ushirikiano wa kutembeleana wakitumia kauli mbiu ya
Pamoja. Miongoni mwa mambo wanayojifunza katika ziara hizo ni uongozi na
maadili yake.
Katika semina hiyo ya maandalizi
iliyoandaliwa na Pamoja kwa ushirikiano na shirika la - The
Konrad-Adenauer-Stiftung (KAS). Miongoni mwa masuala yaliyozungumziwa ni
undeshaji wa uchumi katika muktadha wa soko huria lenye kujali ustawi wa jamii.
Akiongea kwa kujiamini Dk. Kassala alisema
kwamba uchumi wa soko huria usiozingatia jamii ndiyo umeifikisha Tanzania hapa
ilipo kwa sasa ambapo kuna tofauti kubwa ya kipato kati ya watu wachache walionacho
na wananchi walio wengi wasionacho.
Mada tajwa ililenga katika kuangalia wajibu
wa serikali katika kuhakikisha usalama kwa rika la vijana, na kulinda utamaduni
wao bila kuathiriwa na mfumo wa utandawazi.
Bi Debora Maleyek akiuliza swali
Katika mijadala iliyoendeshwa katika mdahalo
huo ilijidhihirisha kwamba vijana wengi
wanakutana na changamoto kubwa mara
wanapohitimu masomo yao kwa sababu ni wachache wanaopata nafasi za kuendelea na
masomo ya juu huku wengi wao wakiwa hawana ujuzi wowote wa kujiajiri au
kukabiliana na changamoto za maisha.
Dk. Kassala anasema kwanza tatizo la Tanzania
siyo uwepo wa sera bali ni sera zilizopo na zimekosa watekelezaji wake. Anasema
kitendo cha vijana wengi kuyakimbia maeneo yao ya asili na kujitafutia ujira wao
katika miji mikubwa ni kiashiria cha kukata tamaa kwa tabaka hilo muhimu katika
jamii.
Anasema vijana ambao bado damu zao zinachemka
huwa wakorofi pale wanapoburuzwa bila kuambiwa ni wapi wanakopelekwa. Na hasa
inapotokea kwamba hawahusishwi katika maaamuzi ya namna ya kuendeshja uchumi.
Dk Kassala anakumbusha kwamba vijana
hawajawahi kuhusishwa katika mjadala wa namna ya kujitafutia mitaji, wala
ubinafsishaji, mizunguko ya pesa katika uchumi na namna mtu mmoja mmoja anavyoweza
kushiriki katika uchumi wa taifa.
Anasema Tanzania imejiwekea malengo kwamba
itakuwa na uchumi wa daraja la kati mara ifikapo mwaka 2025 lakini haoni dalili
zozote zinazoashiria maono hayo. Kwa mfano, ni njia gani zitatumika, katika
ngazi gani? na wahusika wakuu ni akina nani.
Mwanazuoni huyo anasema kwamba maono hayo
yanatakiwa kuwamo katika bajeti ya taifa ya sasa, namna ya kuanzisha ajira,
namna ya kukuza sekta binafsi, namna ya kukuza kilimo ambacho ndiyo uti wa
mgongo wa uchumi wa taifa hili, na namna ya uendeshaji wa taasisi za umma.
Mtaalamu huyu anasema kwa kawaida jamii
imekuwa na tabia ya kutupa lawama kwa vijana bila kuangalia kwamba kabla ya
kukengeuka kwao walikuwa wamejengewa mfumo gani wa kimaadili ambao hautoi
uhakika wa usalama kwao na kutoa uhakika wa maisha yao ya baadaye.
Dk. Kassala anasema vijana wengi huwa na
matumaini ya kupata mafanikio kwa haraka na hilo likishindikina ndipo vijana
hujiingiza katika mambo maovu. Kimsingi anasema vijana wanatakiwa kuoneshwa
kwamba wanakumbukwa na watawala.
Alisema njia nyingine kwa viongozi ni kujenga
mazingira ya kukubalika ni kuzingatia maadili, uhuru, na kujiamini kunakoweza
kuwafanya wajitegemee hata pale wanapokosa ajira.
Anasema Mwl. Nyerere alipotangaza Azimio la
Arusha alilenga kuleta amani, kulinda mali binafsi lakini pia kuweka uwazi na
uwajibikaji katika kusimamia ugavi wa raslimali za umma. Anasema kimsingi
serikali inatakiwa kujenga mifumo ya kuwalinda wananchi wake ambao ndiyo
wazilishaji kiasi kwamba hata wakipata hasara basi waweze kufidiwa.
“Wananchi ni lazima walindwe pale wanapopata
hasara, inabidi tuthamini utu kabla ya faida,” anasema kukosa utu kwa tabaka la
chini ndiko kumesababisha chuki kutokana na watawala kuwajali wawekezaji badala
ya Watanzania.
Mtaalamu huyo anainisha mambo kadhaa ambayo
ya naweza kuisadia Tanzania. Kwanza ni utu, kuheshimu maadili, na tamaduni za
Kiafrika. Anasema serikali inatakiwa kuondokana na dhana ya kuthamini pesa
kuliko utu. 
Bw Deus Fidelis akichangia katika mada hiyo
Vile vile anashauri kwamba jamii iepukane na
tabia ya kuthamini amali za kimagharibi na kuwasahau Watanzania na tamaduni zao.
Anashauri kwamba teknolojia mpya kama ipad na mambo mengine yanayohusisha
mitandao ya intaneti yalenge kwenye mambo ya kujenga na wala siyo kuupotosha
umma.
Nao vijana walipata nafasi ya kutoa michango
ya mawazo na kuuliza maswali na hali ilikuwa kama ifutavyo: Bi Deborah Maleyek
alitaka kujua Azimio la Arusha ni nini kwa nini lilishindwa kufanya kazi
endelevu.
Akijibu hoja hiyo Dk. Kassala anasema kwamba
azimio hilo lilikuja kama jibu muafaka katika kipindi cha mwanzo wa uhuru wa
nchi hii baada ya kutokea misigano ya
kifikra ya namna ya kuendesha utawala wa nchi hii.
Anasema wapo waliotaka kupata mafao kama waliyopata
watawala wa kikoloni kabla ya uhuru huku wengine wakiona kwamba kufanya hivyo
ni kuwadhulumu wanyonge.
“Nyerere aliona kwamba wenzake wanatamaa ya
kuvaa viatu vya wazungu na akatafuta uhalali wa kufanya hivyo na azimio hilo
likawa ndiyo msingi wa kuondokana na wale wasiotaka kujinyima kwa ajili ya
walio wengi” anasema.
Kassala anasema kwamba Mwl. Nyerere
alihakikisha kwamba Watanzania wanapata elimu ya bure katika ngazi zote na
ndiyo maana kulikuwapo na elimu ya watu wazima. Msingi wa kufanya hivyo
ulitokana na imani kwamba uelewa utasaidia katika maendeleo ya kiuchumi.
Lakini anawaeleimisha vijana kwamba miongoni
mwa mambo muhimu aliyoyafanya Mwl. Nyerere ni kuhakikisha kwamba kila Mtanzania
anapata ardhi ambayo inasimamiwa na rais wa nchi.
Akijibu sehemu ya pili ya swali hilo msomi huyo
anasema kwamba siyo kwamba Azimio la Arusha lilishindwa bali mapokeo ya siasa
za kiliberali yalipongia nchini na katika hali ya kurekebisha uchumi baadhi ya
watu wenye ushawishi waliweweseka, na kupotoka kiasi cha kushindwa kuona mazuri
ya azimio hilo.
Naye mwanachuo Kamala Dickson aliomba
kufahamu iwapo kufufuliwa kwa Azimio la Arusha ni jambo linalowezekana katika
hali ambapo uchumi wa soko ndiyo unaotawala.
Akajibu swali hilo Dk Kassala anasema hilo ni
jambo linalowezekana kwa sababu Tanzania inaendeshwa katika mfumo wa uchumi
mchanganyiko uanaozingatia mahitaji ya kibinadamu.
Kwa upande wake Semainda Fredrick alitaka
kujua matokea hasi ya mfumo wa soko ambayo labda Mwl Nyerere aliyahofia katika
enzi za utawala wake. Akijibu swali hilo Dk Kassala anasema kwamba hakuna mfumo
usiokuwa na hitlafu zake lakini kilichokosena ni udhibiti wa serikali baada ya
Mwl. Nyerere kustaafu.
Kwa maana hiyo anasema kwamba uchumi wa
kijamaa bado unakubalika sehemu nyingi mpaka sasa isipokuwa udhibiti wa
serikali hupishana sehemu moja hadi nyingine.
“Nimetembea hadi Venezuela nikashangaa kuona
kwamba chini ya utawaka wa marehemu Hugo Chavez Azimio la Arusha lilitafsiriwa
kwa Kireno ili kila mmoja alifahamu vilivyo kwa hiyo udhaifu haukuwa kwa
nadharia yenyewe bali katika utekelezaji wake.
Lewis Mmbando anauliza iwapo kiwango cha
maendeleo ya sayansi na teknolojia kinaruhusu mfumo wa soko huru kufanya kazi
vizuri. Anasema jambo la msingi ni kukubalika kwa dhana zenyewe kwa Watanzania.
Bi. Agnes Kessy akiuliza swali
4.
Naye Cacilie Radert –akiwakilisha taasisi ya KAS
anasema kwamba historia ya Wajerumani iliwasidia sana katika kuleta maendeleo
ya kiuchumi kwa sababu waliona wana wajibu wa kulinda hadhi ya taifa lao katika
misingi ya uzalendo.
Anasema kitendo cha Ujerumani kutengwa baada
ya vita ya pili ya dunia kiliwafanya wananchi wa taifa hilo kujiuliza wao
wanaweza kuifanyia nini nchi yao. Hata hivyo anasema kwamba changamoto kubwa
iliyokuwapo ni kwamba kulikuwa na uhaba
wa fedha za kuyasaidia makundi yasiyozalisha likiwamo kundi la wazee.
Vile vile Ujerumani ilipata kazi kubwa ya
kupambana na wapinzani wake wa nje lakini pia namna ya kurejesha nguvu ya taifa
katika uzalishaji.
1
3.
Bado nasubiri kwa kina kuona iwapo kweli hapo mwakani 2017 Azimio la Arusha litarejewa
JibuFuta